AVEVA ANENA KUSHUKA KIWANGO CHA MAVUGO - ANGA ZA KIMATAIFA

Latest

Tuesday, October 18, 2016

AVEVA ANENA KUSHUKA KIWANGO CHA MAVUGO

Rais wa klabu ya Simba Evans Aveva, amempa ushauri wa bure mshambuliaji wake Laudit Mavugo kwa kumtaka kupunguza presha ili aweze kufanya vizuri uwanjani.

 Aveva amesema, Mavugo ni mchezaji mzuri lakini amekuwa na papara na uchu wa kufunga mabao na anapokosa mambo humuwia vigumu na kujikuta anashindwa kufanya vizuri awapo uwanjani.

“Tutamtafutia watu wa saikolojia waweze kuongea naye ili aweze kurudi kwenye kiwango chake, tunachojua yeye ni mchezaji mzuri mwenye uwezo mkubwa kama atatulia na kufuata maelekezo ya kocha na asisikilize kelele za mashabiki,” amesema Aveva.

Mavugo alitua kwa mbwebwe kwenye klabu hiyo miezi mitatu iliyopita na kuonyesha uwezo mkubwa ikiwemo kufunga bao kwenye mechi yake ya kwanza ya utambulisho wake dhidi ya AFC Leopard ya Kenya na baada ya hapo alianza kwa kasi mechi za ligi ya Vodacom kwa kufunga mabao matatu katika mechi zilizoongozana lakini baada ya hapo imekuwa kazi bure hajafunga bao katika mechi tano zilizopita na amekua akianzishwa benchi katika mechi mbili za hivi karibuni.

No comments: