YANGA
wameanza rasmi mbio za kutetea ubingwa wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania
Bara – baada ya leo kuwatandika wenyeji Kagera Sugar mabao 6-2 katika
mchezo uliofanyika Uwanja wa Kaitaba, Bukoba.
Ushindi
huo wa kwanza mkubwa zaidi msimu huu, unaifanya Yanga SC ifikishe
pointi 21 baada ya kucheza mechi 10 na kupanda hadi nafasi ya pii, nyuma
ya Simba SC yenye pointi 26.
Katika
mchezo huo uliochezeshwa na refa Suleiman Kinugani aliyesaidiwa na
Ferdinand Chacha na Nicholas Makalanga, hadi mapumziko Yanga walikuwa
wanaongoza 3-1.
Kipindi
cha pili, Kagera wakaanza vizuri na kufanikiwa kupata bao la pili
dakika ya 49, mfungaji yule yule Mbaraka Yussuf aliyetumia makosa ya
mabeki wa Yanga.
Hata
hivyo, Yanga wakaamsha hasira zao na kufanikiwa kupata bao la nne
lililofungwa na Deus Kaseke dakika ya 58 kwa shuti akimalizia krosi ya
Msuva.
Chirwa akaifungia Yanga bao la tano akimalizia mpira uliotemwa na kipa Burhan baada ya shuti la Ngoma.
Donald
Ngoma akakamilisha ushindi mnono wa Yanga leo kwa kufunga bao la sita
dakika ya 64 baada ya kuambaa na mpira na kumchambua Burhan kufuatia
pasi ya Haruna Niyonzima.
Katika mchezo mwingine Azam FC ikiwa nyumbani imepata ushindi wa goli 1-0 dhidi ya JKT Ruvu.
Matokeo ya mechi zote tarehe 22.10.2016:
Sunday, October 23, 2016
Subscribe to:
Post Comments (Atom)


No comments:
Post a Comment